#MaajabuYaKinyonga #Makala #Kinyonga @DailyNewsDigital
Kinyonga ni jamii ya reptilia anayetajwa kuwa ni miongoni mwa viumbe vilivyo na maajabu mengi endapo utaamua kutenga muda wako na kumfuatilia. Nafahamu mtu akitaja kinyonga, harakahara wazo linakujia na kupata picha ya; mnyama anayetembea kwa madaha kuliko hata bishoo wa mtaani kwenu na kujibadilisha rangi mara kwa mara.
Pamoja na hayo, Daily News Digital inaangazia sifa tano za mnyama huyu hivyo baki na mimi, Tagato James Tagato. @DailyNewsDigital